MGOMBEA URAIS WA TFF AKILI KUW YEYE NI MSOMALIA

Kaimu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na mgombea nafasi ya urais wa shirikisho hilo, Wallace Karia akiri kuwa na asili ya Somalia.
Kwa mujibu wa mtandao wa kijamii wa Twitter wa Shirika la habari la Azam TV imeandika kuwa “Nina asili ya Somalia kweli sikatai, lakini hilo ni kabila tu, mimi ni raia wa Tanzania tena wa kuzaliwa – Wallace Karia (Kaimu Rais wa TFF)”.
Julai 01, 2017 kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam imempitisha Wallace Karia kuwa Kaimu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) huku Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi kuwa Kaimu.
Wallace Karia ni miongoni mwa wagombea wa nafasi ya rais wa TFF, huku wengine waliyopo kwenye kinyang’anyiro cha nafasi hiyo ni Jamal Malinzi ambaye kwa sasa anakabiliwa na makosa 28 yakiwemo na utakatishaji fedha, Imani Madega, na Fredrick Masolwa uchaguzi huo unatarajia kufanyika Agosti 12 mwaka huu.

Comments