Fundi cherehani sehem ya 3

FUNDI CHEREHANI
Sehemu Ya 3
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓
"mmmmhhhhh makuuubwa"
"madogo yapo kwenye bukta"
"kwahio sasa"
"niruusu kwanza afu nikakupe mautamu"
"mmmhhhhhhhh"
"mmmhhh nini kwani ni ndugu yako"
"weweee naogopa unaweza kumfanya vibaya mtoto wa watu"
Nesi alizidi kukataa kata kata lakini mbaya zaidi ni kwamba nesi nae kuna kitu anataka kutoka kwa mfanya kazi huyu, yaani huyu nesi anaonekana ni Lesbian ( penzi la jinsia moja)  Nesi alilegezwa na maneno na huyu HouseGirl ili tu aruusiwe kufanya anachokitaka kwangu..
"sawa, ila leo naomba unikune mwenzio"
"we usijali, tena tutaenda kitandani kwangu, maana hata mimi mwenyewe nina hamu"
"kweli fatu"
"kweli vile, sasa nikudanganyie nini"
"basi nenda usichelewe, ila uangalie usije muumiza mgonjwa"
"mmmhhh kwani mwili wangu ni chuma"
"basi nenda"
ENDELEA...........
Nilikua nikiyasikia tu kupitia maskio yangu maana hata jicho sikuwahi kufumbua toka nipate ile ajali mpaka leo hiii sijawai kufungua jicho wala mdomo, kupumua yenyewe natumia mipira, hivyo kuona wanachokifanya ni ngumu, ila kwa kuskia naskia vizuri tu, yaani hata nikiskiskia nachinjwa siwezi kuamka wala kufungua macho,
Sasa baada ya fatu kuruusiwa kuja kwangu, eti anipige tu kiss ndio ataridhika, lakini fatu alipofika nilihisi kushikwa shikwa mithili ya kutomaswa,
Mara nesi akamuita fatu
"we fatu"
"nini wewe"
"bado tu"
"aaaa na wewe"
Fatu alitoka pale nilipo na kumfata nesi kule alipo,
"sio na wewe, toka saa hio hukumaliza tu"
"bado sijamaliza bwana hebu niache kama dakika mbili hivi"
Mara mlango wa chumba hicho ukafunguliwa bila kubisha hodi kwa huyo anaeingia,
"shkamoo boss"
"shkamoo dokta"
"marahaba, vp huyu anafanya nini huku"
"eee, nnneee, naniii, aaaa,.... Alikuja kuniuliza ampikie mgonjwa chakula gani"
"kwanini wewe usitoke badala ya yeye kuingia"
"nisameee dokta"
"sikia nesi, hiki chumba hairuusiwi mtu wa aina yeyote kuingia humu zaidi ya wewe, mama yake na mimi basiiii"
" sawa dokta nimekuelewa"
"na wewe fatu, kuanzia leo staki kuona mtu huku ndani sawa,"
"sawa boss"
"haya toka haraka sana"
Niliskia vishindo vya kukimbia huku mlango ukifungwa kwa hasira, dokta alimuuliza nesi wake kuusu maendeleo yangu,.... Mama nae alifika huku akiwa na shauku ya kuniona kama kuna nafuu kidogo ya kupona kwangu, japo nilidanganyiwa kufa ili kesi niliopewa iishie hewani, na hilo lilikua ni wazo la mama yangu, Japokua hali niliokua nayo haikua tofauti na mfu, maana licha ya kuambiwa mfu, lakini pia afya yangu ilikua mbaya zaidi kuliko kawaida, hivyo hata mtu ukimuambia kua nimekufa lazima aamini kua nimekufa maana hali yangu ilikua mbaya, na mpaka sasa pia hali yangu sio nzuri kabisa
BAADA YA MIEZI MITATU KUPITA
Mungu ni mwema, kwani niliweza kupona ila bado sikua vizuri kiafya ila kutembea angalau kwenda chooni nilikua naenda ila kwa kushikwa mkono, hata kula pia nilikua nakula kidogo,.... mwili wangu ulikonda yaani nilikonda mpaka nilikua najiogopa, yaani ule wembamba wangu wa siku zote umekua mara dufu zaidi, yaani nilikua nimeisha mpaka sura inaonyesha mifupa fupa,
"baba pole"
Alikua ni mama yangu mzazi MWAJABU au ANTI MWAJU ndio aliokua akinipa pole maana toka nilazwe kwenye nyumba hio ya dokta kwa siri mno, hakuwahi kukosa kuja hata siku moja, tena akija hua analia kwa uchungu, kwa kuniona jinsi ninavyoumwa,
"asante,...... shkamoo mamy"
"marahaba ujambo baba"
"aaaa sjambo"
"naona leo kidogo afadhali, maana hata kucheka unacheka, mmhh namshukuru mungu kwakweli"
"ahahahaha aaa ila bado mbavu zinauma uma kiasi"
"usijali mwanangu utapona tuuu"
"asante, afu mamy, simu yangu ipo wapi"
"sadikiii, kwasasa hutakiwi kua na simu baba"
"aaaaa mamy, we nipe tuuu"
"dikiii acha ubishi mwanangu, ila sawa lakini laini yako nimeichoma"
"haaaaaa kwanini mamy"
"kwasasa wewe ni mtu wa siri sana hutakiwi kujulikana"
"kwanini nisijulikane mamy"
"sadiki, nitakuambia pindi utakapo pona kabisa, maana inaonekana hujui kuusu hilo ila kwasasa watu wanajua kua umekufa"
"haaaaaaaa yaani nimekufa mimi"
"diikii mwanangu, wacha niluambie tu ukweli sababu ya wewe kudanganya kifo"
"haaaa aisee hapana, yaani nimekufa mimi"
"sikia sasa, kama unakumbuka kuna kesi ilikupata mwezi wa kumi na mbili mwishoni, lakini kwa bahati mbaya pale pale ukagongwa na toyo, na hali yako ilikua mbaya sana huku ukiwa unatokwa na damu nyingi mno, tulipokuleta hospitalini niliwaza mengi kuusu wewe, kutokana na hio kesi, hivyo niliweza kumfuata dokta na kumwambia kua akupige sindano ya usingizi afu atoe taarifa za uongo kua umekufa ili ile kesi yako iishe, na nilifanya hivyo na ikafanikiwa kweli kesi imefutwa, na namshukuru mungu umepona mwanangu"
"ila mamy umenidanganyia kifo kweli, ila ok anewei je vp ni nani na nani anajua uzima wangu"
"kiukweli hakuna mtu yeyote anaejua zaidi ya mke wako, maana alitaka kunifia mtoto wa watu, kwahio nikamuambia ukweli kua hujafa"
"alitaka kukufia kivipi tena"
"amesema hawezi kuishi bila wewe, bora na yeye afe, sasa nikaona kuliko mtoto wa watu afe, bora niseme"
"Enheeee vp dada aisha anajua uzima wangu"
"hajui, tena analia kila siku akiona picha zako yaani amechanganyikiwa toka aliposikia kifo chako"
"yes, usimuambie kabisa yaan abaki hivyo hivyo"
"kwanini"
"yaani kwa jinsi ninavyomjua dada yangu, aisee usimuambie kabisa"
Nilimuambia mama yangu kua asimuambie dada aisha kua mimi ni mzima, maana dada aisha nilishawahi kutembea nae kimapenzi na aliapa kutokuachana na mimi hata kama ni ndugu, kwahio ndio maana staki ajue kua mimi ni mzima maana atataka tufanye mapenzi na mimi, afu mimi sitaki tena maana nishajua kua ni ndugu yangu, ila yeye hataki kujua hilo kua sisi ni ndugu ila anachotaka ni kuuendeleza uhusiano wangu mimi na yeye
UNAWEZA UKAJIULIZA KUA HUYO DADA YANGU NILIMKULA WAPI,..... HUYO DADA YANGU TULIANZA UHUSIANO KWENYE STORY ILIOPITA, IITWAYO ( "SECONDARY SCHOOL" ) NA NDIO MAANA NAKUAMBIA HUTOIELEWA HII STORY KAMA HUKUISOMA HIO "SECONDARY SCHOOL" KWAHIO NAKUSHSURI NENDA KAISOME HIO AFU UJE UENDELEE NA HIII... MAANA KILA NITAKACHO KIANDIKA HAPA KINATOKA KWENYE HIO STORY, HIVYO KAMA HUKUISOMA, KIUKWELI HII HUTOIELEWA
"mmhhh haya, ila kesho nakuja na mkeo"
"sawa, sasa nipe simu yangu"
"sadikiii nakuomba sana nipo chini ya miguu yako mwanangu, kama kuna namba unaijua kwa kichwa, tafadhali sana naomba uisahau kabisa baba"
"sawa nimekuelewa, ila laini mpya je siruusiwi kuitumia"
"unaruusiwa, na tayari nimeiweka humo, nimekusajiria na kitambulisha changu"
"sawa asante"
"nikuletee chakula gani baba"
"ugali tu"
"ugali na nini,"
"na maarage tu"
"sitaki, nakuletea na nyama na samaki na mnavu sawa"
"pia maarage ueke kidogo"
"inaonekana una hamu nayo"
"hehehehe ndio"
Basi mama yangu aliondoka zake, na dokta wakati huo alikua hayupo, hivyo mama alipoondoka, nilimuona nesi nae anaingia huku akitabasam,
"mambo dikii"
Nesi alinisalimia huku akikaa karibu yangu,
"poa tu"
"simu yako nzuri"
"mmhh asante"
"tubadilishane namba basi"
Nilimuangalia huyu nesi huku nikimshusha juu chini kisha nikamjibu tu kwa ustaarabu,
"mmmhh namba yenyewe hata siijui kwa kichwa"
"lete nijibipu basi"
"mbona kama unaing'ang'ania sana"
"kwani we hujui"
"sijui ndio"
"nataka siku ukiruusiwa, tusiache kuwasiliana"
"apana utanisumbua mbele ya mke wangu"
"jamani dikiii, nipe bwanaaa"
"afu we ni mtu mzima lakini una akili za kitoto"
"kama zako"
"ivi una maana gani kuanza kunirembulia hivyo"
Nilimuuliza huku yeye akiwa amerembua ile mbaya
"kwasababu wewe ni hensam naaaaa unaonekana unayajua, maana nanii yako kubwa"
"afu wewe ni mtu mzima ujue"
"kwani mtu mzima hana tobo"
"ati nini"
"nilisema hivi, ivi sasa hivi mwanamke akivua nguo utamuacha"
Itaendelea.....

Comments